Omba omba mtumia kisu kuomba misaada Iringa akamatwa na Polisi

YULE omba omba maarufu wa mjini Iringa, Mohamed Chengulla anayetumia kisu kuwatisha watu anaotaka wamsaidie fedha amekamatwa na Jeshi la Polisi Mkoa  wa Iringa baada ya msako mkali kufanywa dhidi  yake.

Kijana huyo alikamatwa leo leo majira ya saa 5 asubuhi katika eneo la Posta  mjini Iringa baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa  wananchi, hasa  wanawake ambao  wamedai kufukuzwa mara kwa mara na kijana huyo akiwa na kisu chake mkononi baada ya kunyimwa pesa anazotaka kusaidiwa.


Kamanda  wa Polisi Mkoa wa Iringa, Peter Kakamba pamoja na kuthibitisha  kutokea kwa  tukio hilo ametaka wananchi  kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo pindi wanapoona au kukutana na matukio yanayohatarisha usalama wa mali na maisha yao.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright 2025 EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo