Mvua iliyoambatana na upepo mkali, mawe na radi yasababisha maafa makubwa Butiama.
Kaya zaidi ya 130 zimekosa makazi baada ya nyumba zao zaidi ya 150 kuezuliwa mapaa na nyingine kubomoka kabisa huku zaidi ya ekari 50 ya mashamba ya zao la Mihogo kuharibiwa vibaya kufuatia mvua kubwa ambayo imeambatana na upepo mkali, mawe na radi kunyesha na kusababisha maafa hayo makubwa katika kijiji cha Nyamikoma kata ya Kyanyari wilaya ya Butiama mkoani Mara.





