Neema yawashukia waandishi wa habari wapatao 175

Baraza  la habari  Tanzania  (MCT) limeanza kutoa mafunzo maalumu wa waandishi wa habari yatakayowajengea  uwezo wa  kuandika habari sahihi zinazohusiana na masuala ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi OCTOBA zitakazowapa  wananchi uwezo wa kuwapima wagombea na hatimaye kuchagua viongozi wenye sifa.

Hayo yamesemwa leo na ALAKOK MAYOMBO, afisa program mwandamizi  wa MCT anayeshulikia masuala ya viwango na ubora wakati akielezea madhumuni ya  mafunzo hayo yanayowashirikisha waandishi wa mikoa ya MWANZA, GEITA, SIMIYU, KAGERA na SHINYANGA yatakayochukua siku TANO. 
 
Kwa upande wake mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo, CHRIZOSTOM RWEYEMAMU katika ufunguzi wa mafunzo hayo amewahimiza waandishi wa habari kuandika habari zenye ukweli ili wajiepushe madhara ambayo wanaweza kukumbana nayo

Nao MBEKI MBEKI na ROSE SAMWEL ambao ni miongoni mwa washiriki wa mafunzo hayo wanaoeleza changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo katika kuandika habari zinazohusiana na masuala ya uchaguzi, huku MIDRAJI IBRAHIMU akiwaomba wamiliki wa vyombo vya habari wawawezeshe waandishi ili wajiepushe na vitendo vya uandishi wa habari usiozingatia maadili.
 
Mafunzo hayo yamegawanywa katika mikoa iliyoko kwenye kanda SABA ambapo jumla ya waandishi MIA MOJA SABINI na TANO hapa nchini watanufaika na mafunzo hayo.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo