Clara Mwatuka enzi za uhai wake.
Aliyekuwa Mbunge wa Viti maalumu kupitia Chama cha Wananchi (CUF), Clara Mwatuka, amefariki dunia Jumapili jioni baada ya gari lake alilokuwa akisafiria kupinduka lilipokuwa linashuka eneo la Makonde Plateu kuelekea Ndanda, Masasi mkoani Mtwara.
Gari alilopata nalo ajali marehemu Mwatuka.
Gari ilikuwa inaendeshwa na dereva wake, ambaye inasemekana ni mwanaye.
Mwili wa marehemu Mwatuka umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Ndanda.
Viongozi waandamizi wa CUF wamethibitisha kutokea msiba huo.
wenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. AMEN.
