Kipindupindu chapiga hodi mkoa wa Pwani

Baada ya kushambulia mikoa ya Dar es Salaam na Morogoro, ugonjwa wa kipindupindu sasa umepiga hodi katika Mkoa wa Pwani na tayari watu tisa wameonekana kuwa na dalili za ugonjwa huo.
Hali hiyo imeulazimu uongozi wa idara ya afya mkoani Pwani kutenga maeneo ya kuwalaza kwa ajili ya vipimo na tiba huku katika Mkoa wa Dar es Salaam ugonjwa huo umewakumba watu 348 na vifo 10. Juzi, Mkoa wa Morogoro uliripotiwa kuwa na wagonjwa 32 huku mmoja akiwa tayari amepoteza maisha.
Wakati wagonjwa katika mikoa hiyo wakizidi kuongezeka, Ofisa Afya wa Mkoa wa Pwani, Simon Malulu alisema mtu mmoja amethibitika kuugua kipindupindu huku wengine wanane wakilazwa kwa kuwa na dalili za ugonjwa huo.
Alisema Agosti 18, kulikuwa na wagonjwa wawili kutoka Bagamoyo na wamekuwa wakiongezeka kutoka Mkuranga, Kibaha Vijijini na Kibaha Mjini.
Alisema mara ya mwisho, ugonjwa huo uliikumba Pwani mwaka 2005.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo