SHEHENA YA SUKARI KUTOKA BRAZIL YAKAMATWA TANGA

Mamlaka ya mapato nchini (TRA) tawi la Tanga kwa kushirikiana na kikosi cha polisi majini kimefanikiwa kukamata shehena ya sukari mifuko 254 katika bandari bubu ya Sahare ambayo ilikuwa ikitokea nchini Brazili kupitia Pemba hadi jijini Tanga bila kulipiwa ushuru.

Mkuu wa operesheni wa (TRA) mkoani Tanga Bwana.Kaimukelwa Johansen amesema uchunguzi uliofanywa umeonesha kuna shehena kubwa ya sukari kisiwani Zanzbar iliyotokea nchini Brazili ambayo imekuwa ikisafirsihwa katika baadhi ya mikoa kupitia njia ya panya na bandari bubu ikiwemo mkoa wa Tanga ambayo inauzwa maeneo mengi.
 
Kwa upande wake meneja wa forodhwa mkoani tanga Bwana. Pius Kibahila amesema hii ni mara ya pili kwa sukari kukamatwa kutoka Brazil ikiwemo ile ya awali iliyokamatwa mwezi wa tano mwaka huu hivyo amewaomba wakazi wanaoishi jirani na bandani bubu kutoa ushirikiano kwa kikosi cha polisi cha wanamaji au TRA ili kudhibiti hujuma hizo.
 
Kufuatia hatua hiyo mamlaka hiyo imetangaza vita kwa wafanyabishara wasiokuwa waaminifu kuwa watataifisha vyombo vilivyohusika na hujuma za ukwepaji ushuru wa forodha pamoja na kuchukua hatua kali za kisheria kwa watu wanaofanya makusudi kuzorotesha jitihada za serikali katika zoezi la ukusanyaji wa mapato.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo