Mgombea Ubunge kupitia CHADEMA Zanzibar Bikwao Hamad amefariki dunia muda mfupi baada ya kumaliza kujieleza kwa wapiga kura wake.
Mwenyekiti wa CHADEMA Mjini Unguja Janeth Fusi alisema alianguka ghafla wakati akitoka nje ya ukumbi baada ya kujieleza kwa wapigakura.
Alisema uchaguzi huo wa viti maalum ulikuwa ukifanyika katika makao makuu ya chama hicho.
“Bikwao alikua akitoka nje ghafla tulisikia mtu kaanguka…tulimpatia huduma ya kwanza lakini hali yake iliendelea kuzorota na tukaamua kumkimbiza hospitali na bahari mbaya alifariki dunia” Janeth.
Ripoti ya daktari ilieleza kuwa Bikwao alipata mshtuko wa damu na kumuathiri kichwani na kabla ya kifo chake alipatiwa matibabu katika hospitali ya Al0-Rahma na baadaye kuhamishiwa hospitali ya rufaa ya mnazi mmoja.