Mgombea Ubunge adondoka na kufa papo hapo baada ya kujieleza kwa wajumbe

Mgombea Ubunge kupitia CHADEMA  Zanzibar Bikwao Hamad amefariki dunia muda mfupi baada ya kumaliza kujieleza kwa wapiga kura wake.
Mwenyekiti wa CHADEMA  Mjini Unguja  Janeth Fusi alisema alianguka ghafla wakati akitoka nje ya ukumbi baada ya kujieleza kwa wapigakura.
Alisema uchaguzi huo wa viti maalum ulikuwa ukifanyika katika makao makuu ya chama hicho.
“Bikwao alikua akitoka nje ghafla tulisikia mtu kaanguka…tulimpatia huduma ya kwanza lakini hali yake iliendelea kuzorota na tukaamua kumkimbiza hospitali na bahari mbaya alifariki dunia” Janeth.
Ripoti ya daktari ilieleza kuwa  Bikwao alipata mshtuko wa damu na kumuathiri kichwani na kabla ya kifo chake alipatiwa matibabu katika hospitali ya Al0-Rahma na baadaye kuhamishiwa hospitali ya rufaa ya mnazi mmoja.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo