Jeshi la polisi mkoani simiyu kwa kushirikiana na kikosi maalum cha
askari wa hifadhi ya taifa ya Serengeti wamefanikiwa kumkamata
mtuhumiwa wa ujangili bw madeni nindwa mkazi wa kijiji cha mwalukonge
wilayani busega aliyekamatwa na meno ya tembo yenye thamani shilingi
milioni 17,baada ya kutoroka na hatimaye kukamatwa katika kijiji cha
makomero wilayani igunga alikokuwa amejificha.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kaimu kamanda wa polisi mkoa wa simiyu ssp jonathan shana amesema kuwa kesi hiyo ilifunguliwa ,katika mahakama ya wilaya ya magu ec2/2014 mbele ya hakimu masige ambapo iliendeshwa siku tatu mfulilizo kuanzia,desemba 2 hadi desemba 5,2014 na kumalizika kusikilizwa na mtuhumiwa alijitetea januari,8,2015 na kubaki hukumu dhidi yake.
katika mazingira ya kutatanisha mtuhumiwa januari 13 mwaka huu, alitolewa gerezani kwa removal order iliyosainiwa na hakimu aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo bila kuwepo kwa wakili mwandamizi mfawidhi wa wa serikali .
Shana amesema jalada la uchunguzi limefunguliwa kupata ukweli wa mazingira kwa mtuhumiwa kuachiliwa mahakamani huku akitoa wito kwa wananchi.
Mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakama ya wilaya ya magu ,juni 22 ili kujulishwa hukumu iliyotolewa dhidi yake.
Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari kaimu kamanda wa polisi mkoa wa simiyu ssp jonathan shana amesema kuwa kesi hiyo ilifunguliwa ,katika mahakama ya wilaya ya magu ec2/2014 mbele ya hakimu masige ambapo iliendeshwa siku tatu mfulilizo kuanzia,desemba 2 hadi desemba 5,2014 na kumalizika kusikilizwa na mtuhumiwa alijitetea januari,8,2015 na kubaki hukumu dhidi yake.
katika mazingira ya kutatanisha mtuhumiwa januari 13 mwaka huu, alitolewa gerezani kwa removal order iliyosainiwa na hakimu aliyekuwa akiisikiliza kesi hiyo bila kuwepo kwa wakili mwandamizi mfawidhi wa wa serikali .
Shana amesema jalada la uchunguzi limefunguliwa kupata ukweli wa mazingira kwa mtuhumiwa kuachiliwa mahakamani huku akitoa wito kwa wananchi.
Mtuhumiwa huyo anatarajiwa kufikishwa mahakama ya wilaya ya magu ,juni 22 ili kujulishwa hukumu iliyotolewa dhidi yake.
