BASI LA NGOMUO LAPATA AJALI MBAYA YA KUPINDUKA MARA TATU HUKO SINGIDA

Watu wawili mkoani Singida wamekufa na wengine zaidi ya ishirini na tano wamejeruhiwa kwa kuvunjika mikono na miguu katika ajali mbili tofauti  zilizo husisha basi na lori na nyingine mwendesha pikipiki  kugongwa na lori.

Akieleza kamanda wa polisi mkoani Singida ACP Thobiasi Sedoyeka amethibitisha kutokea kwa ajali hizo ambazo zimehusisha basi la Ngumuo lenye usajili wa namba T 476 CSH aina ya yutong lilikuwa likitokea Moshi na kuelekea Kahama na lori namba T 343 DCP lenye tela namba T 936 DBY lilokuwa likitokea mwanza na kuelekea Dar-es-Salaam na kusema kuwa zimesababishwa na mwendokasi wa dereva wa basi na uzembe wakati akiendesha.
 
Wakielezea jinsi ajali ilivyo tokea majeruhi wamesema dereva wa basi lao alikuwa akiendesha kwa mwendo wa kasi huku mvua ikinyesha na ghafla wakaona basi lao linayumba na kugongwa na tela la lori kisha likapunduka mara tatu.
 
Kwa upande wake mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Singida Daktari Daniel Tarimo amesema wamepokea maiti mbili na majeruhi ishirini na sita ambao wamesha patiwa matibabu na wengine itabidi wapewe rufaa ya kwenda hospitali KCMC na Muhimbili kwa sababu wamevunjika vibaya.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo