PROF. LIPUMBA NA BAADHI YA WANACHAMA WAKE WAKAMATWA NA POLISI


TAARIFA zilizotufikia ni kwamba Mwenyekiti wa CUF, Prof Ibrahim Lipumba na wanachama wake wamekamatwa na kupigwa na Jeshi la Polisi.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimeeleza kushtushwa na tukio hilo la kupigwa na kukamatwa Mwenyekiti Mwenza wa UKAWA Prof. Lipumba.

Uongozi wa juu wa Chadema pamoja na mawakili wa chama hicho wameelekea Kituo Kikuu cha Polisi, Dar kwa ajili ya tukio hilo walilofanyiwa viongozi hao wa CUF na wanachama.

Juhudi za Mtandao huu kumpata Kaimu wa Kamanda wa polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamanda Suleiman Kova, Afande Sirro zinaendelea baada ya kumpigia simu hapo awali na kuomba kupigiwa baadaye kutokana na kikao alichokuwa nacho.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo