Madansa wa Staa wa Bongo Fleva, Diamond Platinum wamekamatwa leo na wapo
Kituo cha polisi cha Oyster Bay, Dar kwa kuvaa sare za JWTZ.
Wakati huohuo polisi wanaendelea kumtafuta bosi wao, Nasibu Abudul '
Diamond Platinumz' kwa mahojiano naye kwa kuvaa sare za Jeshi hilo
katika Tamasha la Serengeti Fiesta, lililofanyika Leaders Club, Dar
usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita.
Tutawajuza zaidi kinachoendelea
(HABARI NA MUSA MATEJA/GPL)