KILICHOTOKEA UWANJANI KWENYE MECHI YA YANGA NA SIMBA UWANJA WA TAIFA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh1VhFZGIDisMHDcZH3qQRoGBftpbZF7VLpWAzz47GiBh0yhCH83TWb00ii6Ppy2N8EYYeHm__K2hxj2fEAJ1tQkJ0VKEWwGtdbIor4JDz4R49InahrrThDP3opIh6gluhcgPmAWQWd6I25/s1600/2.jpg
Mchezo namba 27 wa Ligi Kuu ya Vodacom uliowakutanisha watani wa jadi Young Africana kutoka eneo la Jangwani na Simba SC kutoka eneo la msimbazi jijini Dar es salaam umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana (0-0), mtanange uliofanyika jioni ya leo kwenye dimba la Uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Young Africans ilingia uwanjani chini ya kocha wake Marcio Maximo kusaka pointi tatu hali kadhalika Phiri wa Simba akisaka alama tatu pia hali iliyopelekea mchezo huo kuwa mgumu kutikisika kwa nyavu za pande zote mbili.

Kocha mbrazil alimtumia mshambuliaji Jaja akisaidiwa na Coutinho, Ngasa, Niyonzima na viungo Mbuyu Twite na Hassan Dilunga huku Phiri akimtumia Maguri kama mshambuliaji kiongozi akisaidiwa na Kiemba, Ndemla, Chanongo na Okwi.

Young Africans ilifanya mashambuizi kadhaa langoni mwa Simba kupitia kwa washambuliaji wake hali kadhalika wapinzani nao walifanya hivyo pia lakini mashambulizi ya timu zote mbili yalikuta yakiishia mikononi kwa walinda mlango wa timu zote.

Mpaka dakika 45 za kipindi cha kwa kwanza zinamalizika, Young Africans 0 - 0 Simba SC.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko kwa lengo la kusaka bao la mapema katika mchezo wa huo, lakini kutokua makini kwa washambuliaji wa timu zote kulifanya milango kuendelea kuwa migumu kufunguka.

Andrey Coutinho alikosa nafasi mbili za kuipatia Young Africans bao baada ya kupokea krosi nzuri ambazo alishindwa kuzitumia vyema kuukwamisha mpira wavuni na kukuta michomo yake ikiokolewa na mlianda mlango wa Simba SC Manyika Peter.

Simba ilifanya mashmabulizi langoni wa Young Africans kupitia kwa washambuliaji wake Okwi, Maguri na Chanongo lakini jitihada zao hazikuzaa matunda na kukuta mipira yao ikiishia mikononi wa mlinda wa Deo Munish "Dida" na mingine kupaa juu ya lango au kuokolewa na walinzi.

Mpaka dakika 90 za mchezo zinamalizika, Young Africans 0 - 0 Simba SC.

Young Africans: 1. Dida, 2. Juma Abdul/Telela, 3. Oscar, 4. Cannavaro, 5. Yondani, 6. Twite, 7.Dilunga, 8.Niyonzima/Msuva, 9.Jaja/Kizza, 10.Ngasa, 11. Coutinho

Simba SC: 1. Manyika, 2. Gallas, 3. Mohamed, 4. Isihaka, 5. Owino, 6.Mkude/Seseme, 7.Chanongo, 8/Ndemla/Kisiga, 9.Maguri, 10.Kiemba/Messi, 11.Okwi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo