skip to main |
skip to sidebar
DEREVA AMSHUSHIA KIPIGO KIBAKA ALIYENASA MLANGONI MWA BASI HUKU AKIENDESHA, ANGALIA VIDEO HAPA
Katika kituko hiki kilichotokea katika jiji la Concepción, nchini
Chile, huyu kibaka, alipodaiwa nauli mara baada ya kuingia kwenye basi,
alimwambia dereva kuwa hana nauli, na kuwa mmoja wa abiria ni shangazi
yake (kitu ambacho si kweli.) Kisha akaanza kutoa visingizio kibao,
akisubiri nafasi ya kukwapua pochi.
Dakika ya mwisho, wakati basi linaanza kufunga mlango, alijaribu
kukwapua mkoba wa mwanamke aliyekaa siti ya mbele. Bahati nzuri
alishindwa kuiba mkoba huo, halafu alichelewa kutoka nje ya basi na
kunaswa na mlango uliokuwa unajifunga. Hapo ndipo dereva alipotoa rungu
lake na kuanza kumpa kichapo huku akiendelea kuendesha basi.
Kibaka huyo aliendelea kula kichapo huku akijitetea au kuomba
msamaha, mpaka basi liliposimama mbele ya askari polisi, na askari huyo
kumtia mbaroni. Taarifa zaidi zinasema kuwa kibaka huyo ana historia ya
uhalifu, na kwa sheria za nchi hiyo, ambazo ni kali kwa wahalifu
wanaorudia makosa, ataishia jela.
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi