ANGALIA HII VIDEO ALICHOFANYIWA BAADA YA KUMSHIKA MCHEZAJI MAKALIO UWANJANI

Muamuzi Manuel Zeleya ameingia katika lindi la lawama kutoka kwa wachezaji pamoja na viongozi wa klabu ya Marathon inayoshiriki ligi kuu ya nchini Honduras, kufuatia adhabu ya kadi nyekundu aliyompa mlinda mlango wa klabu hiyo.


Viongozi pamoja na wachezaji wamekuwa wakimlalamikia muamuzi huyo kufuatia maamuzi mazito aliyoyachukua, na kupelekea kikosi chao kicheza pungufu.


Muamuzi Zeleya alichukua jukumu la kumuadhibu mlinda mlango wa klabu ya Marathon, Junior Morales wakati wa mchezo wa ligi uliowakutanisha na Real Sociedad, kutokana na utovu wa nidhamu aliouonyesha wa kumshika makalio kwa makusudi mchezaji wa timu pinzani.


Hata hivyo muamuzi huyo hakuona kosa hilo, mpaka pale aliposhtuliwa na msaidia wake namba mbili, na katika hali ya mshangao alichukua maamuzi ya kumuonyesha kadi nyekundu Junior Morales na mwisho wa mambo aliamuru mkwaju wa penati kupigwa kwenye lango la Marathon.


Wakati maamuzi hayo yanachukuliwa tayari timu hizo zilikuwa zimefungana bao moja kwa moja.


Katika picha za televisheni Junior Morales ameonekana akimshika makalio mshambuliaji wa Real Sociedad, Morales kwa makusudi baada ya kuumiliki mpira uliokuwa unaambaa ambaa kwenye lango lake.


Hata hivyo Henry Martinez aliechukua jukumu la kupiga mkwaju wa penati kufuatia maamuzi yaliyochukuliwa na Manuel Zeleya, alikosa na hivyo kuufanya mchezo huo kumalizika kwa matokeo ya sare ya bao moja kwa moja.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo