Mchungaji mmoja wa kanila Anglican amejikuta matatani baada ya kubambwa
uchi kitandani na mke wa mtu, ambaye ni mmoja wa waumini wake jijini
Nairobi, Kenya.
Mume wa mwanamke huyo akiwa amejawa na hasira,
anaonekana akimpa kichapo mkewe; huku mchungaji huyo, mwenye pete ya
ndoa mkononi kuashiria kuwa ana mke, akivaa nguo zake taratibu.
Alipoulizwa kulikoni, mchungaji huyo alitoa kisingizio kuwa mwanamke
huyo alimuomba aende hotelini hapo kumfanyia maombi.
Kuongeza msumari wa
moto kwenye kidonda, mchungaji na mume wa mwanamke huyo ni marafiki wa
muda mrefu.
Cha ajabu, mchungaji na mume huyo walionekana wakiondoka
eneo la tukio pamoja kuelekea kwenye magari yao.