Mwenyekiti Wa CHADEMA Atinga Makao makuu ya Jeshi la Polisi Kuhojiwa huku akisindikizwa na Wanachama wake.....Vurugu Zaibuka, wananchi watawanywa

Baadhi ya wapenzi na wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), wakishangilia baada ya gari lililokuwa limembeba Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, alipowasili leo Makao Makuu wa Jeshi la Polisi jijini Dar es Salaam, kwa mahojiano.

Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), wakimpa kichapo mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, Josephat Isango, nje ya Makao Makuu ya Polisi, Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA John Mnyika akizungumza na waandishi wa habari waliokuwepo kwenye eneo la makao makuu ya Jeshi la Polisi,juu ya kile kilichokuwa kikiendelea kwenye mahojiani katika ya Mwenyekiti wa Chama hicho na Jeshi la Polisi.

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Freeman Mbowe akiwasili kwenye makao makuu ya Jeshi la Polisi nchini,Mapema JANA asubuhi tayari kwa kwenda kuhojiwa juu kauli aliyoitoa kwenye Mkutano Mkuu wa chama hicho hivi katibuni,kuwa watafanya maandamano nchini nzima bila kikomo.

Makamu Mwenyekiti wa Chadema,Prof. Abdallah Safari na Wakili wa Chama,Wakili Mabele Marando wakiwasili kwenye Makao Makuu wa Jeshi la Polisi mapema JANA.

Baadhi ya Wachama na Wafuafi wa Chadema wakishangilia wakati Mwenyekiti wao akiwasili kwenye Makao Makuu ya Jeshi la Palisi.

Ulinzi mlali katika eneo hilo.
Askari akiwataka wanachadema kuondoka.
Huyu alikuwa akikaidi amri ya Jeshi la Polisi ilibidi aondolewe kwa nguvu.

Mmoja wa wanachama wa CHADEMA mbaye jina lake halikuweza kupatikana, akipewa kibano na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU), nje ya Makao Makuu ya Polisi, Dar es Salaam.

Ulinzi mkali.

Mwenyekiti wa Chama cha DP, Christopher Mtikila akihojiwa na askari Polisi, alipowasili Makao Makuu ya Polisi jijini Dar es Salaam kwa kutumia usafiri wa bajaji, ambako Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe alihojiwa na Polisi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo