Zaidi ya wanafunzi 2,178
wamemaliza mitihani ya kuhitimu
elimu ya msingi wilayani Makete mkoani Njombe katika
hali ya utulivu na amani
Mitihani hiyo iliyoanza hapo jana katika shule zote za msingi nchini kwa zaidi ya wanafunzi 808,11 kuanza mitihani
hiyo nchi nzima huku katika wilaya ya Makete wanafunzi walio fanya mtihani ni 2,178 wavulana wakiwa 1,045 na wasichana wakiwa
1,133 na wamemaliza hii leo bila
kuripotiwa vitendo vya udanganyifu wala dosari
Idadi hiyo ni tofauti na mwaka uliopita ambapo zaidi ya wahitimu 844,938 walifanya mtihani huo nchi nzima
Eddy blog imetembelea katika vituo vya mtihani na kushudia
hali ya utulivu na wanafunzi wakiwa katika vyumba vya mtihani huku ulinzi
ukionekana kuimarishwa jambo ambalo limesaidia mtihani hiyo kuendelea kufanyika hadi mwisho bila matatizo
Kwa upande wao wazazi na walezi wamepongeza idara ya elimu kwa kusimamia
mitihani hiyo na kuomba walimu wanaopewa dhamana ya kusimamia wawe wazalendo kwa kuto jihusisha na udanganyifu wakati wa mitihani hiyo katika kipindi kijacho
Mapema wiki hii Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi,
Jenister Mhagama alizitaka kamati za mtihani mikoa na wilaya kusimamia ipasavyo kuepuka vitendo vitakavyopelekea mitihani kufutwa ama kuahirishwa.
