MEYA JERRY SILAA AMLILIA IGP MANGU KUHUSU ASKARI WAKE

MEYA wa Ilala, Jerry Silaa amemuomba Mkuu wa Jeshi la Polisi Ernest Mangu kutokubali askari wake kuwa wakala wa sheria za barabara.
 
Silaa alisema hayo katika uchaguzi wa Naibu Meya uliofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

Alisema askari wengi wanajichukulia sheria mkononi kwa kuwakamata baadhi ya madereva kwa madai kuwa magari yao yamezidi viwango hivyo yanaharibu barabara pasipo kuzingatia sheria.

Pia Silaa ameitaka Mahakama ya Jiji kuacha kuwakamata wananchi kwa makosa yasiyofaa na ambayo hayana uhakika, kuwatoza faini zisizo na msingi na kuwaweka mahabusu bila hatia.

“Ninapigiwa simu na kupewa malalamiko mara kadhaa wananchi wanaonewa bila sababu za msingi na kuwafanya wajione sawa na wakimbizi katika nchi hii,” alisema Silaa.

Pamoja na hayo alisaini mkopo wa sh bilioni 1.2 kutoka Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) kwa ajili ya kununua magreda mawili ya kutengeneza miundombinu ya halmashauri.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo