Baadhi ya silaha zilizokamatwa na jeshi la polisi.
Kamanda Suleiman Kova akionyesha silaha zilizokamatwa kwa wanahabari (hawapo pichani).
Baadhi ya wanahabari wakimsikiliza Kova.
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam
linamshikilia mtu mmoja anayefahamika kwa jina la Gunner Meena (40)
mkazi wa Kinyerezi, Segerea, Dar es Salaam, kwa tuhuma za kujifanya
mtumishi wa Idara ya Usalama wa Taifa .
Tukio la mwisho lililomfanya akamatwe ni pale alipomtishia
mfanyabiashara mwenye asili ya Kisomali aitwaye Abdi Dalmar, ili ampe
Tshs 25,000,000/= ama sivyo angechukua hatua chini ya Sheria ya Usalama
wa Taifa.
Aidha jeshi hilo katika kuendesha oparesheni zake za kutokomeza
ujambazi wa kutumia silaha limefanikiwa kukamata bastola nne na
shot-gun moja wiki hii.
Na Gabriel Ng’osha/GPL
JIUNGE NA EDMO BLOG SASA
Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube
Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi