WATUHUMIWA WATANO WALIOMLAWITI MTOTO WA KIUME KUANZA KUJITETEA MAHAKAMANI WILAYANI MWANGA

MAHAKAMA ya Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro, imewakuta na kesi ya kujibu watuhumiwa watano wanaoshitakiwa kwa tuhuma za kulawiti mtoto wa kiume wa miaka 16 (jina linahifadhiwa) ambaye ni mwanafunzi wa Shule ya Sekondari J.K Nyerere wilayani humo.

Watuhumiwa hao ni Charles Kiule maarufu kama Nguto, January Alhaj na Patrick Sapisi, wakiwemo walimu wawili; Hadija Salum na Namwaka Mbwana wote waliokuwa wakifundisha katika Shule ya Sekondari J.K Nyerere ambao watapadishwa kwa mara nyingine kizimbani Julai 2, mwaka huu, kwa ajili ya kuanza usikilizaji wa kesi hiyo.

Washitakiwa hao walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Emmanuel Njuu ambapo
ilielezwa kuwa mshitakiwa wa kwanza hadi wa tatu ambao ni Nguto, January na Patrick wanakabiliwa na kosa la kulawiti.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa Novemba 3 mwaka jana, saa 12 jioni katika eneo la Lembeni, Wilaya ya Mwanga, washitakiwa hao kwa pamoja walimwingilia kinyume na maumbile mwanafunzi huyo na kisha kumuingizia karoti na matango katika sehemu zake za haja kubwa halafu wakamlazimisha kula matunda hayo.

Washitakiwa hao pia wanakabiliwa na kosa la pili la kujeruhi, ambapo ilielezwa mahakamani hapo kuwa kabla ya kutekeleza kosa la kwanza, walimpiga kijana huyo kwa kutumiwa waya wa umeme na fimbo hali iliyomsababishia maumivu makali mwilini.

Katika kesi hiyo namba 118 ya mwaka 2013, washitakiwa namba nne na tano; Hadija na Mbwana ambao wote ni walimu katika shule hiyo, wanakabiliwa na kosa la kuwashawishi washitakiwa namba moja, mbili na tatu kufanya kitendo hicho.

Ilidaiwa mahakamani hapo kuwa walimu hao waliwashawishi washitakiwa kumfanyia kitendo hicho cha kinyama kama kulipa kisasi kwa kile kilichodaiwa kuwa mwanafunzi huyo alitaka kumbaka mtoto wa mwalimu wake (Hadija).

Upande wa mashitaka ukiongozwa na mwendesha mashitaka wa serikali, Beatus John, uliwasilisha mashahidi nane huku upande wa utetezi, mshitakiwa wa kwanza hadi wa tatu walijitetea wenyewe na wakili Rehema Mtulya anawatetea washitakiwa wa nne na tano.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo