
Mkuu wa Kitengo cha Polisi cha Kupambana na Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa
---
Raia wa Nigeria, Anthony Ifeanyichukwa Okafor (52), amekamatwa
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere akidaiwa kumeza kete 100
za dawa za kulevya aina ya cocaine ambazo thamani yake bado
haijafahamika.
Tukio hilo limetokea takribani siku 22 baada ya
raia mwingine wa Nigeria, Olabisi Ibidun Cole (65) kuvunja rekodi ya
umri wa watu wanaokamatwa wakiwa na dawa za kulevya katika uwanja huo.
Cole alikamatwa Jumatatu ya Mei 19, mwaka huu saa
tisa alasiri akijiandaa kwenda Paris, Ufaransa kwa ndege ya Shirika la
Ndege la Ethiopia, akiwa amemeza kete 82 aina ya heroini zilizokuwa
zimefungwa kwenye karatasi zinazofanana na ganda la sigara, ambazo si
rahisi kuonekana katika mitambo.Kwa habari zaidi Bofya na Endelea.......