KIJANA AUAWA BAADA YA KUVAMIA NYUMBA NA KUMCHARANGA MAPANGA MWANAMKE

Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Jumanne Joel(25-30) ameuawa na wananchi wenye hasira kali baada ya kumvamia Monica Lutonja(32)  wa kijiji cha Nyankumbu katika kata ya Kalangalala mjini Geita .
 
Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana ambapo inadaiwa kuwa watu watatu akiwemo marehemu walienda kwa mama huyo na kugonga hodi wakidai kuwa wao na rafiki wa kaka yake ambaye ni Bunegezi.

Baada ya Monica Lutonja kufungua walianza kumkatakata mapanga sehemu mbalimbali za mwili wake hadi kupoteza fahamu.
 
Hata hivyo kelele za mama huyo zilisababisha majirani kutoka na kuanza kuwasaka baada ya kuwa wamekimbia na hatimaye wakamkamata mmoja na wakaanza kumpiga hadi kumuua.
 
Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Joseph Konyo amethibisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa  watuhumiwa wengine wawili bado wanatafutwa na jeshi la polisi kwa ajili ya kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Na Valence Robert-Malunde1 Blog- Geita


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo