HII NI VIDEO NYINGINE INAYOTABIRIWA KUFUNGIWA HIVI KARIBUNI, INAITWA MFALME WA MAPENZI, ITAZAME HAPA

June 9 ilitoka rasmi video ya wimbo wa msanii wa kike wa Kenya aitwae Sanaipei, unaoitwa Mfalme wa Mapenzi na ndani ya siku mbili tu uliangaliwa YouTube zaidi ya mara 59,000.
Video hiyo iliyoongozwa na Mhando Brian imetabiriwa kufungwa isichezwe kwenye vituo vya television vya Kenya kwa kuzingatia kilichotokea kwa wimbo wa Sauti Sol, Nishike.
 
Mfalme wa Mapenzi inawezekana imeenda nje ya maadili hata zaidi ya video ya wimbo wa Nishike wa Sauti Sol kwa kuzingatia vigezo vilivyotajwa hadi kuifungia hiyo Nishike.
 
Sanaipei anaonesha jinsi ambavyo anaweza kupata faraja ya moyo kutoka kwa mwanaume anaejua wapi pa kushika na nini cha kufanya wanapokuwa faragha. 

Hilo linaweza lisiwe tatizo, lakini tatizo linaweza kuwa jinsi alivyoonesha kwa vitendo na hisia kuhusu kile anachokizungumzia.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo