Serikali imetoa siku tano kwa mamlaka ya mapato (TRA) na COSOTA kukaa pamoja na kutengeneza stika za kukusanya ushuru pamoja na za kulinda wizi wa kazi za wasanii.
Naibu waziri wa fedha na uchumu Mh. Mwigulu Nchemba ametoa agizo hilo bungeni Dodoma hii leo wakati akijibu swali la Nyongeza la mbunge wa viti maalum Mh Martha Mlata.
Mh. Mwigulu amesema si kweli wasanii na kuona kuwa kazi zao hazina maana, bali imekuwa ikijitahidi kutambua kazi zao na wao wanufaike na jasho lao na ndiyo maana ametoa agizo hilo.
Mh Mlata alikuwa akilalamikia kuwepo kwa stika za TRA ambazo hukusanya ushuru tu lakini hakuna ukusanyaji mzuri wa stika unaonufaisha wasanii.
Na Edwin Moshi, Dodoma
