LINAH ATANGAZA KUFUNGA NDOA HIVI KARIBUNI

Stori: Musa Mateja, GPL
MSANII mwenye sauti mwanana anayetesa kwenye Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’, amefunguka kuwa, ndoa yake na mpenzi wake Nagari Kombo ‘Kaka wa Bongo’ inanukia.

Linah alisema hayo wikiendi iliyopita aliponaswa akijiachia na Kaka wa Bongo katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambapo mpango mzima wa Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013 – 2014 ulikuwa ukifanyika.
Lina akiwa na mpenzi wake huyo ambaye ni mume.

“Sina haja ya kuendelea kumficha mpenzi wangu, kwani kwa sasa anatambulika kwa kila mtu na hasa ndugu zangu wa karibu, kitu cha kusubiriwa kwa sasa ni tarehe ya ndoa yetu tu,” alisema Linah.

Kaka wa Bongo alijizolea umaarufu siku za nyuma baada ya kuingia uwanjani na kumkumbatia mchezaji, Ricardo Kaka wa Timu ya Taifa ya Brazil iliyokuwa ikichuana na Taifa Stars katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo