Wafanyakazi
wa Hoteli ya Sharon iliyopo Ubungo jijini Dar es Salaam wagoma
kuendelea na majukumu yao ya kila siku huku kisa kikielezwa kuwa ni
kutolipwa mshahara wao wa mwezi Aprili.
Habari
kutoka eneo la tukio zinasema, mgomo huo umefanyika ikiwa ni baada ya
wafanyakazi hao kujiunga na chama cha wafanyakazi kiitwacho Chadau
jambo linalopingwa na uongozi wa hoteli hiyo.
