OKWI AONDOKA KIMYAKIMYA KWENDA KWAO UGANDA

Emmanuel Okwi akisubiri wapambe wake waliombebea mizigo huku simu ikiwa sikioni akiongea na mtu.
Wapambe (nyuma)  na Okwi akiwa mbele wakielekea ndani ya uwanja wa ndege sehemu ya abiria wanapopumzika.
Mwandishi wa gazeti la Mwanaspoti, Khatimu Naheka, akimbembeleza Okwi aongee naye lakini mchezaji huyo aligoma akimwambia hataki kuongea naye chochote.
Okwi huyo akiondoka!
Naheka alikuwa hajakata tamaa, aliendelea kumbembeleza tena lakini pia hakufanikiwa.
Okwi akiingia ndani ya uwanja kwa ajili ya ukaguzi.
…Akitafuta hati yake ya kusafiria.
Mlinzi  akikagua hati yake.
Okwi akienda kupanda ndege.

MCHEZAJI wa timu ya Yanga, Emmanuel Arnold Okwi,  jana usiku alipanda ndege na kuondoka kwenda kwao nchini Uganda.

Mchezaji huyo alifika uwanjani hapo majira ya saa moja usiku akiwa ameongozana na wapambe wake ambao hawakutambulika majina yao mara moja.

(Picha/habari: Shakoor Jongo /GPL.)


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo