Liverpool leo wameheza kandanda safi ingine kwa miaka kibao kwa kuichabanga Manchester United 3-0 katkauwanja wao wa nyumbani wa Trafford on
Sunday, huku mkongwe asiyezeeka Steven Gerrard akitikisa nyavu mara mbili kwa njia ya penati na kulihamasisha Bwawa la Maini kwa mara ingine tena.
Kiungo huyo alipiga penati mbili za kufa mtu kuhakikisha vijana wa Brendan Rodgers wakiondoka na pointi
tatu zote.
Luis Suarez aliongeza maumivi kwa Man U baada ya ‘chumba’ cha uhakika cha Daniel Sturridge kilipoguswa na kudondoka mbele yake, ambapo raia huyo wa Uruguay hakufanya makosa alipochomeka kitu nyavuni mbele ya kipa wa Man U David De Gea kumaliza kazi ya siku.
Ndio kusema Bwawa la Maini limechukua tena nafasi yake pili (kuelekea ya kwanza) baada ya kuikopesha Manchester City kwa masaa kadhaa. Hadi sasa, kwa mujibu wa wataalamu wa soka, hakuna sababu ya kulifanya Bwawa la Maini likose kunyakua ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa mara ya 20!