WANANCHI WENGI WAJITOKEZA KUPIGA KURA KATIKA UCHAGUZI JIMBO LA KIEMBESAMAKI


Wananchi Jimbo la Kiembesamaki, Zanzibar wakiangalia majina yao kujua vituo vyao walivyopangiwa kupiga kura leo asubuhi.

Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
HABARI kutoka Zanzibar zinasema uchaguzi mdogo wa uwakilishi Jimbo la Kiembesamaki kisiwani humo unaendelea vizuri na wapiga  kura wengi wamejitokeza kwenda kutimiza haki yao ya kimsingi.
 
Ulinzi umeimarishwa katika vituo vya kupigia kura.
Mwandishi wetu wa huko anasema jana kulikuwa na malumbano ya hapa na pale kwa wanachama wa vyama viwili vikubwa vya siasa, Chama Cha Mapinduzi (CCM)  na Chama Cha Wananchi (CUF), kwani walikuwa wakitambiana kila upande ukidai utashinda katika kinyang’anyiro cha leo.
Tutakuwa tukiendelea kuwapasha yanayotokea.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo