WABUNGE WAKUNWA NA HIFADHI YA GOMBE KIGOMA


Baadhi ya watalii wakiwa eneo la hifadhi ya Gombe.

Na Ojuku Abraham
WABUNGE ambao ni wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Ardhi, Maliasili na Mazingira, wamekunwa na kitendo cha Mamlaka ya Hifadhi za Taifa (TANAPA) kupitia hifadhi yake ya Gombe mkoani Kigoma, kujenga vyumba vinne vya madarasa ya Shule ya Sekondari ya Kagongo.

Makamu mwenyekiti wa kamati hiyo, Mheshimiwa Abdulkarim Shah alitoa pongezi hizo hivi karibuni kufuatia ziara yao katika hifadhi hizo za taifa zilizo pembezoni mwa Ziwa Tanganyika.

Akizungumza kutoka mkoani Kigoma kwa njia ya mtandao, Meneja Mawasiliano wa TANAPA, Pascal Shelutete, alisema Kamati hiyo ilitembelea hifadhi hiyo na kujionea vivutio vingi vya utalii, ambavyo endapo vitasimamiwa na kuendelezwa, vinaweza kuchangia ongezeko la pato la taifa.

Wajumbe hao waliopokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TANAPA, Allan Kijazi walitembelea sehemu mbalimbali ikiwemo msitu mnene uliopo ndani ya hifadhi hiyo pamoja na maporomoko ya maji ya Kakombe.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo