SIMBA YAITANDIKA JKT OLJORO MABAO 4-0

Mabao matatu ya Amisi Tambwe na moja la Jonas Mkude yamewafanya wekundu wa Msimbazi waondoke na pointi zote tatu uwanja wa taifa dhidi ya JKT Oljoro. 

Ramadhan Singano "Messi" amezidi kuthibitisha ubora wote kwa kupika mabao matatu mchezo wa leo. Jonas Mkude alikuwa wa kwanza kuliona lango la JKT oljoro kufuatia kona ilivyochongwa na Ramadhan Singano, huku dakika ya 24 Amisi Tambwe akifunga kufuatia pande la Singano. 

Dakika ya 28 Tambwe aliziona nyavu za Oljoro kufuatia mpira wa kutanguliziwa toka kwa Singano na kufanya hadi mapumziko Simba waongoze 3-0. 

Kipindi cha pili Amisi Tambwe alijihakikishia kuondoka na mpira uwanjani kufuatia krosi ya Awadh Juma. Simba sasa inatimiza pointi 30 ikiwa ni moja nyuma ya Mbeya City ambao wanashikilia nafasi ya tatu wakiwa na pointi 31.

Matokeo mengine ni:

Ashanti United 0-2 Mgambo Shooting


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo