MWILI wa aliyekuwa mwanahabari wa BBC aliyeaga dunia wiki hii Anne Virginiah Waithera umechomwa katika eneo la makaburi ya umma la Lang'ata mjini Nairobi.
Lilikuwa ombi
la Anne aliyekuwa anapenda sana kutunza mazingira kuwa mwili wake
uchomwe na kisha majivu yake yatupwe kwenye mto na mengine kuwekwa
katika eneo ambako kutapandwa mti kama kumbukumbu kwake.
Kabla ya
kuchomwa kwa mwili, kuliandaliwa ibada ya wafu katika kanisa Katoliki la
St Paul’s Chapel, lililoko kando ya barabara ya University Way,
Nairobi.
Anne, mwanawe
Bi Jane Wanjiku, na aliyekuwa na umri wa miaka 39 alifariki Januari 27
baada ya kuugua saratani ya ubongo kwa miaka miwili tangu mwaka 2012.
Aliwahi
kufanya kazi na mashirika mawili makuu ya habari nchini Kenya, Nation
Media Group ambapo alifanyia kazi kituo cha redio cha Easy FM na Royal
Media Services ambapo alifanyia kazi kituo cha televisheni cha Citizen
kabla ya kujiunga na shirika habari la Uingereza, BBC.
Katika BBC,
alikuwa anafanya kazi kama ripota wa redio na televisheni hasa
alipokwenda Ethiopia, kama ripota wa kwanza mwenye uwezo wa kuripoti
katika lugha mbili, Kiswahili na Kiingereza.
Mchapa kazi
Ndiye
mwanahabari wa pili mashuhuri wa BBC kuaga dunia mwezi huu baada ya
Komla Dumor aliyesifika kutokana na makala yake ya redio ya Focus on
Africa kufariki kutokana na mshtuko wa moyo akiwa Uingereza.
Wakuu wa
idhaa ya BBC Swahili David Okwemba, Ali Saleh na mkuu wa BBC Afrika
Solomon Mugera wamemtaja Ann kama mchapa kazi na na mfanyakazi
aliyependa kujituma na kwamba BBC imepoteza mwanahabari mahiri sana
Afrika