KATIBU MKUU WA CCM,NDUGU KINANA AKUTANA NA WAENDESHA BODA BODA


 Katibu Mkuu wa Chama cha CCM,Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia waendesha Bodaboda ambap wameonekana kufurahia sana mkutano huo uliofanyika leo ukumbi wa Mtenda,Soweto jijini Mbeya.
 Waendesha Bodaboda kutoka sehemu mbalimbali jijini Mbeya,wakiwa wamembeba Katibu Mkuu wa CCM mara baada ya kuzungumza nao mapema leo jioni ndani ya ukumbi wa Mtenda,Soweto mkoani Mbeya.
 Waendesha Bodaboda kutoka sehemu mbalimbali jijini Mbeya,wakiwa wamembeba Katibu Mkuu wa CCM mara baada ya kuzungumza nao mapema leo jioni ndani ya ukumbi wa Mtenda,Soweto mkoani Mbeya.
 Baadhi ya Waendesha boda boda wafurahia jambo kwenye mkutano huo
Waendesha Bodaboda wakifuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana na Katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye wakati wa mkutano huo.
Katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi,Nape Nnauye akizungumza wakati wa mkutano na Waendesha Bodoboda kutoka sehemu mbalimbali jijini Mbeya leo.
Katibu Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akisalimiana na Inspekta Isack Lema ambaye ni Mlezi wa Bodaboda Mkoani Mbeya,kwa upande wa jeshi la Polisi wakati alipowasili kwenye ukumbi wa Mtenda uliopo Soweto mjini Mbeya kwa ajili ya kuzungumza na Waendesha Bodaboda wa mjini humo,ambapo Wamemweleza matatizo mbalimbali wanayokumbana nayo na jinsi wanavyoshirikiana na jeshi la Polisi na Polisi Jamii katika kulinda Usalama wa Wananchi,wao wenyewe na mali kwa ujumla ,Changamoto mbalimbali za kimaendeleo zimetatuliwa na zitaendelea kutatuliwa ili waendesha bodaboda wafanye kazi zao kwa ufanisi na Utulivu.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo