MASOGANGE ASEMA "NAOGOPA MUME WA MTU"

Na Imelda Mtema
VIDEO Queen mwenye figa matata Bongo, Agnes Jerald ‘Masogange’ amesema anaogopa kama ukoma kutembea na mume wa mtu kama wafanyavyo baadhi ya watu.
Agnes Jerald ‘Masogange’.
Akizungumza na paparazi wetu, Agnes ambaye hivi sasa amejiingiza kwenye soko la filamu, alisema anaogopa sana kuingia kwenye uhusiano na mume wa mtu ndiyo maana anaona bora aendelee na mpenzi wake wa siku zote kuepuka uhasama.
“Sina tabia ya kushobokea kabisa waume za watu,  bora niendelee na mtu wangu wa siku zote na kama tukishindwana basi bora nitafute mwingine lakini awe wangu peke yangu,” alisema Masogange.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo