DJ wa kituo cha radio maarufu kwa burudani nchini Uingereza kilicho
chini ya shirika la habari la Uingereza, BBC cha BBC Radio 1Xtra, DJ
Edu, amemtaja Diamond Platnumz, miongoni mwa wasanii watano wenye dalili
za kufanya vizuri barani Afrika mwaka 2014.

Sio Diamond Plutnumz Pekee aliyetawa bali wasanii wengine waliotabiriwa
kufanya vizuri Afrika ni pamoja na Kaysha,(msanii wa DRC aishie
Ufaransa), Wyre wa Kenya, Radio na Weasel wa Uganda na King James wa
Rwanda.
