Mke
wa Rais na Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo, WAMA,
Mheshimiwa Mama Salma Kikwete akipokea tuzo ya Uongozi Uliotukuka
kimataifa (Global Inspirational Leadership Award 2013) kutoka kwa
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi
Mheshimiwa Bibi Furo Giami, mwishoni mwa mkutano wa siku tatu wa
Wanawake kutoka Afrika, Mashariki ya Kati na Asia. Mkutano huo
ulioandaliwa na Kituo cha Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi (CELD),
wakishirikiana na CEO Clubs Network na African Leadership Magazine
uliofanyika katika hoteli ya Atlantis The Palm, huko Dubai , Umoja wa
Falme za Kiarabu (UAE.) Tuzo hiyo imetolewa tarehe 18.12.2013.
Mke wa Rais Mama Salma Kikwete akitoa hotuba ya kushukuru mara tu baada ya kupokea Tuzo hiyo huko Dubai
Mkurugenzi
Mtendaji wa Kituo cha Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi (CELD), Bibi
Furo Giami akikabidhi vyeti kwa Wake wa Marais na wanawake wengine
waliotunukiwa tuzo hizo wakati wa kilele cha mkutano wa wanawake kutoka
Afrika, Mashariki ya Kati na Asia uliofanyika huko Dubai, Umoja wa Falme
za Kiarabu
Dr. Angela Moore, Balozi wa Hisani kutoka kutoka Jimbo la Georgia, nchini Marekani akiwavisha nishani washindi wa Tuzo .
Wake
wa Marais kutoka Barani Afrika waliotunukiwa Tuzo na Kituo cha
Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi wakionyesha tuzo,nishani na hati
walizokabidhiwa kwa washiriki wa mkutano wa wanawake kutoka Afrika,
Mashariki ya Kati na Asia na wageni wengine waliohudhuria sherehe ya
utoaji tuzo hizo huko Dubai
Wake
wa Marais kutoka Barani Afrika waliotunukiwa Tuzo na Kituo cha
Maendeleo ya Kiuchumi na Uongozi wakionyesha tuzo,nishani na hati
walizokabidhiwa kwa washiriki wa mkutano wa wanawake kutoka Afrika,
Mashariki ya Kati na Asia na wageni wengine waliohudhuria sherehe ya
utoaji tuzo hizo huko Dubai.Picha na John Lukuwi





