Na Gladness Mallya, GPL
STAA wa filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameeleza chanzo cha wasanii Bongo kuigiza mapenzi kwenye filamu ni kwa sababu Tanzania hakuna uhuru wa kuigiza.
STAA wa filamu za Kibongo, Vincent Kigosi ‘Ray’ ameeleza chanzo cha wasanii Bongo kuigiza mapenzi kwenye filamu ni kwa sababu Tanzania hakuna uhuru wa kuigiza.
Akizungumza hivi karibuni jijini Dar, Ray alisema msanii anapoonesha
kipaji chake kwa kuigiza kitu kwa ajili ya kuelimisha jamii anarudishwa
nyuma kwani wakati mwingine inafikia hatua ya filamu husika kufungiwa.
“Hapa Tanzania hakuna uhuru wa kuigiza kama zilivyo nchi nyingine
ndiyo maana kila siku tunaigiza mapenzi tu. Niliwahi kutoa filamu ya
Second Wife (Mke wa Pili), Waislam hawakunielewa mpaka baadaye.
Juzikati nilitaka kutoa filamu ya Sista Maria, Wakatoliki wameipinga
isitoke, sasa nini kimebaki, ni kuigiza filamu za mapenzi tu,” aliema
Ray.