Cheti cha uhitimu wa mafunzo wa udereva wa Pikipiki.
WAHITIMU
wa mafunzo ya udereva mkoani Iringa, wamepatiwa Pikipiki za bure kwa lengo la
kuimarisha ulinzi shirikishi usalama barabarani na kwa kundi hilo ambalo limekuwa likilalamikiwa kutofuata
sheria za usalama wa barabara na hivyo kusababisha ongezeko la ajari.
Akikabidhi
msaada wa Pikipiki mbili katika ukumbi wa Hallfear kwa uongozi wa chama cha waendesha Bodaboda mjini Iringa,
mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na usalama mkoani Iringa Bw. Salim Abri “Asas”
amesema msaada huo ni utekelezaji wa ahadi yake kwa chama hicho cha waendesha
Bodaboda, pekipiki ambazo zitatumika katika dolia.
Bw.
Salim amesema msaada huo ni katika kutambua umuhimu kazi hiyo ya udereva wa Pikipiki ambao kwa
kiwango kikubwa umetoa ajira kwa kundi kubwa la vijana nchini.
Salim
amesema kamati yake ya ulinzi na usalama barabara itahakikisha ajira hiyo
inakuwa salama kwa kutoa elimu kwa madereva wa pikipiki kwa lengo la kupunguza
ajali na vifo vitokanavyo na usafiri huo.
Aidha
wahitimu hao 100 wa mafunzo ya udereva wamelipiwa ada ya elimu hiyo ya udereva huku
mwenyekiti huyo akitoa nafasi nyingine kwa madereva 100 ambapo pia wartapatiwa
elimu hiyo.
Hata
hivyo Bw. Salimu ameahidi kuongeza msaada wa Pikipiki nyingine mbili ili
kuifanya kazi hiyo ya dolia kwa uhakika na kufanikisha mpango wa kutokomeza
ajali na vifo vitokanavyo na usafiri huo wa pikipiki., huku akiwataka madereva
hao kutobweteka kwa kuishia kazi hiyo ya udereva wa Pikipiki bali kufanya
jitihada za kusonga mbele.
“Sidhani
kama kazi hii ya udereva wa Pikipiki mtafanya hata muwapo wazee, cha msingi
mnachopaswa kukifanya ni kuwa na mawazo ya kusonga mbele muwe madereva wa
magari, msiishie hapa kwenye kazi hii ya bodaboda tu!! Lakini ipo haja ya
kuanzisha Saccos yenu ili muweze kukopeshana fedha na kuweza kumiliki Pikipiki
zenu, maana ninaambiwa kuwa hapa baadhi yenu Pikipiki hizi siyo zenu,” Alisema
Salim.
Mkuu
wa kitengo cha usalama barabarani kupitia jeshi la Polisi (OCD) SP Panfil Honono amewataka madereva hao kuwa
na nidhamu katika kazi hiyo na kusimamia sheria za barabarani bila shuruti ili ajira
hiyo iwe na thamani katika jamii.
Naye
mwakirishi wa Kamanda wa jeshi la Polisi mkoani Iringa SP Zakaria Benard
amewataka madereva hao kujihami katika kazi hiyo, kwa kufanya kazi hiyo kwa
umakini mkubwa ikiwa pamoja na kuacha tamaa ya kuwachukua abiria wanaowatilia
shaka.
“Mtu
kama humfahamu siyo lazima umpeleke anakotaka, lakini pia muwe makini kwa
kuwatambua wateja wenu, muulize jina huku ukimuhoji baadhi ya maswali, ambavyo
yatakuwa ni msaada kwako, kitu kingine ndugu zangu!! Acheni tamaa, mfano
unakuta mteja humfahamu anakukodi umpeleke kituo kimoja, unafikanae katika
kituo kile alichosema nataka kufika, anasema umpeleke mbele zaidi, hapo utambue
kuwa huyo siyo abiria mwema, kataa na kisha muache hapo na urudi katika kituo
chako, tunafahamu kumekuwa na wimbi la utekaji na hata mauaji mnafanyiwa kwa
kutumia njia hizo za kuwakodi ili wawapole pikipiki, kwa hiyo hapo kuweni
makini na waangalifu sana,” alisema SP Zakaria.
Na Oliver Motto, Iringa