Wananchi wa kaya zaidi ya 30 za kata ya mto wa mbu
wilayani Monduli mkoani Arusha hawana makazi baada ya mvua
zilizoambatana na upepo mkali kuezua nyumba zao.
Mkuu wa wilaya ya Monduli Bw Jowika Kasunga amesema
mvua hizo pia zimesababisha uharibifu mkubwa katika shule ya sekondari
ya Manyara, jengo la hotel na gari moja mali ya shirika la hifadhi za
taifa Tanzania Tanapa ambalo limeangukiwa na ukuta.
Wakizungumzia tukio hilo wananchi walionusurika
katika mkasa huo ambao asilimia kubwa wamehifadhiwa na kwa ndugu na
jamaa zao pamoja na kuelezea madhara waliyopata wameiomba serikali na
wasamaria wema kujitolea kuwasaidia.
Akizungumzia uharibifu katika shule ya sekondari ya
Manyara mkuu wa shule hiyo amesema wanafunzi wanne wamepata majeraha
madogo na sehemu kubwa ya majengo imeathirika msaada wa haraka
unahitajika.
Eneo hilo wa mto wa mbu ambalo liko kwenye ukanda
wa bonde la ufa limekuwa likikubwa na majanga mbalimbali yakiwemo ya
upepo mkali na mafuriko jambo linaloonyesha kwamba iko haja ya mamlaka
zinazohusika kuchukua tahadhari zaidi hasa ikizingatiwa kuwa idadi ya
watu wanaohamia na kuweka makazi inaongezeka siku hadi siku kwa mujibu
wa maelezo ya mkuu wa wilaya hakuna mtu aliyepoteza maishakatika tukio
hilo
CHANZO:ITV
