FUMANIZII!!!! MKE AMSHIKA UGONI MUMEWE.....MKE ATOKA SAFARI AWAFUMA KITANDANI KWAKE...SOMA ZAIDI MKASA HUU

Usaliti! Recho Mathias (23) anadai kumshika ugoni mumewe wa ndoa akiwa na mwanamke ndani ya chumba chake tena kitandani. 

Recho Mathias aliyemshika ugoni mumewe.

Tukio hilo lilitokea wikiendi iliyopita maeneo ya Mashiri, Mabatini mkoani hapa ambapo Recho alirejea kutoka safarini na kumkuta mumewe anasaliti ndoa yao na mwanamke mwingine aliyedai kuwa ni mke wake halali.

Habari zilidai kuwa baada ya Recho kukutana na hali hiyo chumbani kwake, moja kwa moja alitoa taarifa kwa viongozi wa serikali ya mtaa ambao walishirikiana na wanaharakati wa jinsia wa FARIJIKA katika ‘kusovu’ ishu hiyo.

 
Mume wa Recho aliyeshikwa ugoni akiwa na mwanamke.

Kama kawaida, makamanda wa OFM walijiridhisha kwanza kama kweli mwanaume huyo ni mume wa ndoa wa Recho.

Ilibainika kuwa kweli ni wanandoa ambapo katika kipindi kifupi cha mwezi mmoja ambacho Recho alikuwa safarini kumuuguza bibi yake, mumewe alichukua mwanamke mwingine kwa makubaliano ya kufunga ndoa.

 
Mwanamke aliyenaswa na mume wa mtu.

Baada ya kunasa tukio zima, OFM ikiwa sambamba na Recho, balozi wa mtaa na balozi kiongozi aliyejitambulisha kwa jina la Musa Mohamed, walifika eneo la tukio na kumshuhudia mwanamke mwingine wa mwanaume huyo aliyejitambulisha kwa jina la Salha Hassani akiwa amelala chumbani bila wasiwasi.

Salha alipoulizwa kama anatambua kuwa mwanaume huyo ana mke alishangaa na kusema kuwa hakuwa akijua chochote zaidi ya kusikia uvumi mtaani.

 
Recho Mathias (kushoto), kulia ni mwanamke aliyemshika ugoni akiwa na mumewe.

Huku akiwa na jazba, Recho alifunguka kuwa kinachomuumiza zaidi kuhusu mwanaume huyo siyo kitendo cha chumba chake kutumiwa na mwanamke mwingine bali ni mali ambazo wamechuma wote huku kiasi kikubwa zikiwa zake.

Naye mwanaume huyo alipobanwa na OFM alikataa.

 
Mwenyekiti wa mtaa (kulia) akiwa eneo la tukio. Kushoto ni mume wa Recho.

Kuhusu madai ya mkewe kutaka kugawana mali walizochuma, mwanaume huyo alisema atajitahidi kumlipa huku akiomba suala hilo lisifike mbali badala yake apewe muda.

Hata hivyo, suala hilo lilipelekwa katika baraza la usuluhishi la serikali za mtaa ambapo Recho na mumewe wanatarajiwa kuitwa leo (Jumatatu)  kwa ajili ya kusikiliza shauri lao huku taratibu za kisheria za kushikwa ugoni zikifuatia.


-GPL VIA OFM


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo