Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mkoa wa Iringa Bi. Jesca Msambatavangu, akifanya uzinduzi wa hafla ya
kukabidhi Usafiri wa Pikipiki 125 kwa Chama cha akiba na mikopo, Vijana
Sacco's - ya Vijana wa Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa.
Bi.
Jesca Msambatavangu akitoa ushauri kwa vijana hao, kuacha kubweteka juu
ya hatua hiyo ya usafiri wa Pikipiki, ambapo amewataka kuwa na mawazo
ya mbele zaidi kwa kujipanga kuwa na magari.
"Pikipiki peke yake hazitoshi, haya
chukua na hela hizi shilingi Laki tano zisaidie kuukuza mfuko wa Sacco's
yenu vijana, ninawapenda sana vijana wanaojituma, nyinyi kwa mpango huu
ni rafiki zangu sana sasa," Alisema Msambatavangu.
Viongozi wa CCM Wilaya ya Mufindi wakiwa katika hafla ya kukabidhi Pikipiki 125 kwa 'Vijana Sacco's".
Bw. Felix Lwimbo mwenyekiti wa CCM
Wilaya ya Mufindi akiwa na Bw. Edmund Ngalawa katika hafla hiyo ya
kukabidhi mkopo wa Pikipiki kwa vijana.
"Tunasikiliza maelekezo ya viongozi wetu"PICHA NA OLIVER MOTTO