Wakala wa bara bara mkoa wa Arusha
wamefanya operesheni ya kushitukiza kukagua magari ya mizigo
yaliyozidisha uzito na kugundua idadi kubwa ya magari yaliyozidi uzito
katika mzani wa mpaka wa Namnga huku baadhi ya magari yakiwa yamezidisha
zaidi ya tani thelasini na madereva wake kuyatelekeza na kukimbia
kusikojulikana.
Akizungumza katika operesheni hiyo mkuu wa kitengo
cha mizani mkoa wa Arusha Emanuel Mwakyusa amesema operesheni hiyo
imefuatia kuongezeka kwa magari yanayoongeza uzito na kwamba tangu
kutolewa kwa agizo la waziri mkuu Mizengo Pinda la kuwataka wamiliki
kukaa na serikali kutatua tatizo la ongezeko la tozo za uzito baadhi ya
wamiliki wamekuwa wanatumia vibaya nafasi hiyo.
Kwa upande wao baadhi ya madereva wa magari hayo
wamesema hali hiyo inasababisha na ubovu wa mizani kwani kila mzani
unasoma tofauti huku mizigo ukiwa ni uleule na kuwepo kwa upendeleo wa
magari kutoka nje na wengine wakipongeza hatua ya kutoza faini magari
yaliyozidisha uzito.
Akizungumzia hali hiyo meneja wa wakala wa barabara
mkoa wa Arusha mhandisi Deusidedit Kakoko amesema tuhuma zinazohusu
ubovu wa mizani siyo za kweli bali madereva uongeza mizogo wakiwa njiani
na kama kuna wenye uwakika wa tuhuma zake bado kuna nafasi ya kukata
rufaa kupinga adhabu aliyepewa.