MAJANGILI WAANZA KUUA NDEGE AINA YA TAI KWA KUWAWEKEA SUMU KWENYE MIZOGA YA TEMBO, KISA WANAKIHEREHERE

White-backed vultures poisoned at an elephant carcass.  Photo courtesy of Gonarezhou Transfrontier Park


Mauaji ya tembo yanayoendelea katika nchi mbalimbali barani Afrika yamefikia katika kiwango cha kutisha 'at a point of no return' na ubaya kila kukicha majangili wanakuja na mbinu mpya za kuhakikisha wanatekeleza azma yao.

Baada ya kugundua kuwa wale ndege tai wanatoa taarifa kwa askari wa wanyama pori, (tai wakiona mzoga huwa wanazunguka maeneo hayo) wameanza kuwaua ndege hao kwa kuwawekea sumu katika mizogo ya tembo.


Tai ambao hupenda kuambaa ambaa angani wakizunguka eneo palipo na mzogo wameonekana ni kero na watibuaji wakubwa wa njama za majangili ambao hufanya shughuli zao mchana kweupe.

Elephant felled by poachers.  Photo courtesy of Gonarezhou Transfrontier Park

Tai hukusanyika katika makundi makubwa ili kuweza kupata chakuala kwa kupambana na wanyama kama simba, fisi nk, na kama hali hii itaendelea kuna hatari hata wanyama wengine wala nyama wakiwemo akina fisi, nao wakapoteza maisha.

Katika tukio moja lililotokea huko Botswana tai zaidi ya 600 walikufa baada ya kula sumu iliyowekwa kwenye mzoga wa tembo, hata hivyo hakuna uhakika kama mmlaka zetu hapa nchini zinataarifa ya mauaji haya ya tai katika hifadhi zetu nchini
 
chanzo:tabianchi


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo