Mganga mkuu wa serikali Dr Donan Mmbando akifungua kampeni ya awamu ya pili ya Tupo wangapi ? Tulizana
............
MGANGA mkuu wa
serikali Dr Donan
Mmbando amevipongeza vyombo
vya habari nchini Tanzania kwa jitihada
kubwa za kuelimisha
jamii kupitia kampeni ya
Tupo wangapi? TULIZANA awamu ya
kwanza.
Dr Mmbando
ametoa pongezi hizo
leo jijini Dar es Salaam
wakati wa ufunguzi
wa awamu ya pili ya kampeni ya
TUPO WANGAPI? TULIZANA awamu ya
pili.
Mbali ya pongezi hizo
bado ametaka wanahabari nchini
kuendelea kutoa ushirikiano katika
kuelimisha jamii dhidi ya
kampeni hiyo.
Alisema kuwa
tafiti zinaonyesha kuwa mahusiano
ya
kingono kwa kuwa
na wapenzi wengi ni chanzo kikuu cha VVU
Kwani alisema asilimia
zaidi ya
24 watu waliopo katika ndoo wamekili
kuwa na mahusiano ya kingono asilimia 4 ya wanawake
waliopo katika ndoa wamekili kuwa na mahusiano ya
mpenzi zaidi ya mmoja
Alisema upo
uwezekano wa mtandao
wa ngono kuendelea
kukuwa zaidi iwapo
watu hawatatulizana kwa
kuwa na mpenzi mmoja ambae ni mwaminifu.
Matokeo ya
utafiti wa viashiria
vya malaria na UKIMWi vinaonyesha
kuwa kasi ya
maambukizi ya VVU
ni kubwa zaidi
kwa kuwa na asilimia 5.5
Upo uwezekano wa
kupunguza maambukizi ya VVU
kwa kutulizana kwa
kuwa na mpenzi mmoja
mwaminifu .
Awamu ya kwanza na kampeni hii
imeonyesha mafanikio makubwa baada ya
wasanii kutunga nyimbo mbali
mbali pia taasisi
mbali mbali zimepata kuweka mabango na vielelezo mbali mbali vinavyohamasisha jamii
kuepuka na mtandao wa ngono.
“Utafiti wa kufuatilia
mwenendo wa kampeni hizo
umeonyesha asilimia 71
wamekili kuona jitihada
hizo hivyo awamu ya
pili wizara ya
afya na ustawi wa jamii imepania kuongeza kasi
zaidi ikiwa ni pamoja na
kutumia vyombo mbali mbali
vya habari..tunapenda
kupongeza wanahabari nchini
kutokana na kuendelea kutoa elimu kwa jamii
hivyo ni mategemeo yetu kuendelea
kuelimisha zaidi jamii.”
Dr Mmbando alisema
serikali itaendelea kubuni
mbinu mbali mbali za
kuelimisha jamii juu ya
kampeni hii bila kuwatisha
wananchi .
Pia alisema kuwa kampeni
hii serikali itahakikisha
inawafikia wananchi wote
hata wale waliopo
pembezoni kwa ngazi ya wilaya
hadi kijiji huku akisisitiza
kuwa magari ya
sinema ambayo yapo
wilayani yatatumika kutoa elimu
zaidi.