Mwenyekiti wa jukwaa la katiba nchini Tanzania Bw Deusi Kibanda
akitoa mada katika tamasha la 11 la mtandao wa jinsia Tanzania
(TGNP ) leo katika viwanja vya TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam
Wakati huo huo Katibu wa jumuia ya Wanawake na watoto( SHIVYAWATA) Rebecca Eliazar ameeleza changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu Eliazar alisema kuwa ukatili kwa wanawake walemavu umekuwa mara mbili ya ule wanaofanyiwa watu wa anina nyingine kwani wamekuwa wakidharauliwa huku wakionwa kuwa wao hawana hata haki ya kueza kuzaa na kua na familia.
”Watu wamekua na tabia kuona kuwa ukifanya tendo la ndoa na Mlemavu wa kike unaweza kutoa nuksi au kupata utajiri wa haraka na kuheshimiwa katika jamii”, Alisema Rebecca Eliazar katika warsha hiyo.
Pamoja na mambo mengine katika Warsha hiyo Eliazar aliendelea kusema kuwa huduma mbovu wanazopatiwa walemavu katika vituo vya Afya si rafiki na watu wa jamii hiyo hasa katika suala zima la vitanda kuwa juu na hivyo kupata shida kupanda.
Alindelea kusema kuwa Lugha chafu za dharau kwao pamoja na matusi pia vimekuwea mstari wa mbele wa watu hao hali ambayo inawapa wasiwasi hata wanapopata matatizo ya kuugua,.
Hata hivo Eliazar alisema kuwa watu wakikuona Mlemavu umepata ujauzito wanakutolea lugha mbaya ikiwa ni pamoja na dharau kna kwamba mlemavu wa kike hana haki ya kupata mtoto au kumiliki familia.
“Ukiwa mjamzito ukipishana na watu utasikia watu wanasema kuwa kuwa,
Mwangalieni huyu hajioni hali yake halafu anabeba ujauzito kwanza aliyekupa mimba mimba ni nani?”, Aliongeza Rebecca Eliazar.
Kwa upande wake Mwezeshaji kutoka katika Shirika la Plan Internation
Anna Mushi alisema kuwa mfumo wa kutopata Elimu ya afya ya uzazi kwa watoto ndio chanzo kikubwa cha mimba za utotoni.
Pia Mushi katika Warsha hiyo aliataka wanawake kuwa na amri juu ya miili yao hasa katika suala zima la uzazi hali ambayo itapunguza umasikini katika familia zao na kuchangia haraka shughuli za maendeleo.
Bw Kibanda akisisitiza jambo katika tamasha hilo la TGNP leo
Baadhi ya washiriki wa tamasha hilo wakifuatilia hotuba ya Bw Kibanda leo
Mwenyekiti wa jukwaa la katiba Bw
Deusi Kibanda akitafsili lugha ,wakati mshiriki wa tamasha la TGNP
kutoka nchini Uganda wakati akichangia kuhusu rasimu ya katiba ya
Tanzania
WAKATI mchakato
wa rasimu ya katiba
ukiendelea ,mwenyekiti wa jukwaa
la katiba Deusi Kibanda amewataka wanawake
nchini kutokubali kuipigia kura rasimu
ya katiba mpya
iwapo maoni mbali mbali
yaliyotolewa na wanawake hasa masuala
ya usawa wa
kijinsia yasipoingizwa katika
rasimu hiyo.
Akitoa
mada juu ya mchakato
wa katiba ya Tanzania kwenye tamasha la 11 la mtandao wa
kijinsia Tanzania (TGNP) leo
,Kibanda amesema kuwa asilimia
zaidi ya 70 wapiga kura nchini ni wanawake
hivyo maoni ya wanawake
kama hayatasikilizwa na kuwekwa
mambo ambayo hayamtetei mwanamke
na motto katika rasimu
hiyo ya katiba basi wanawake
nchini wasikubali kuipigia
kura .
Kwani alisema
mbali ya tume hiyo ya katiba kuwa na
wanawake ndani yake ila bado
kwa sehemu kubwa
wameonyesha kushindwa kupigania maoni ya
wanawake kuingia katika rasimu
hiyo ya katiba.
Kibanda alisema
kuwa wakati mchakato
huo ukielekea kufika
mwisho kwa kuwa katika
hatua ya mabaraza la katiba kupitia rasimu
hiyo ya katiba ila
yamekuwepo mapungufu mbali mbali
katika rasimu hiyo baada ya
maoni mbali mbali yaliyotolewa
na wanawake kutoingizwa
katika rasimu hiyo.
Hivyo
alisema kama tume ya katiba itaendelea
na msimamo wake wa
kutoingiza maoni sahihi ya wananchi
katika rasimu hiyo watambue
kuwa hatua ya mwisho
baada ya bunge la katiba
ni wananchi kuipigia kura katiba hiyo
jambo ambalo wananchi wanapaswa kuwa makini na kama itakuwa kimya
bila kuingiza masuala ya usawa wa kijinsia .
Bw
Kibanda alisema kuwa katiba
nzuri ni ile ambayo itayatazama makundi yote
katika hali ya usawa
wa asilimia 50 kwa 50 vinginevyo katiba
haitakuwa na maana kama itakumbatia
mfumo dume na rasilimali za nchi zikawanufaisha wachache .
“
Mchakato huu wa
rasimu ya katiba unaendelea
ila bado ukitazama vema unaona bado katiba imempa mamlaka makubwa
zaidi Rais ya kuteua badala ya kupeleka mamlaka hayo kwa
bunge ambalo ni sauti ya wananchi”
Wakati huo huo Katibu wa jumuia ya Wanawake na watoto( SHIVYAWATA) Rebecca Eliazar ameeleza changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu Eliazar alisema kuwa ukatili kwa wanawake walemavu umekuwa mara mbili ya ule wanaofanyiwa watu wa anina nyingine kwani wamekuwa wakidharauliwa huku wakionwa kuwa wao hawana hata haki ya kueza kuzaa na kua na familia.
”Watu wamekua na tabia kuona kuwa ukifanya tendo la ndoa na Mlemavu wa kike unaweza kutoa nuksi au kupata utajiri wa haraka na kuheshimiwa katika jamii”, Alisema Rebecca Eliazar katika warsha hiyo.
Pamoja na mambo mengine katika Warsha hiyo Eliazar aliendelea kusema kuwa huduma mbovu wanazopatiwa walemavu katika vituo vya Afya si rafiki na watu wa jamii hiyo hasa katika suala zima la vitanda kuwa juu na hivyo kupata shida kupanda.
Alindelea kusema kuwa Lugha chafu za dharau kwao pamoja na matusi pia vimekuwea mstari wa mbele wa watu hao hali ambayo inawapa wasiwasi hata wanapopata matatizo ya kuugua,.
Hata hivo Eliazar alisema kuwa watu wakikuona Mlemavu umepata ujauzito wanakutolea lugha mbaya ikiwa ni pamoja na dharau kna kwamba mlemavu wa kike hana haki ya kupata mtoto au kumiliki familia.
“Ukiwa mjamzito ukipishana na watu utasikia watu wanasema kuwa kuwa,
Mwangalieni huyu hajioni hali yake halafu anabeba ujauzito kwanza aliyekupa mimba mimba ni nani?”, Aliongeza Rebecca Eliazar.
Kwa upande wake Mwezeshaji kutoka katika Shirika la Plan Internation
Anna Mushi alisema kuwa mfumo wa kutopata Elimu ya afya ya uzazi kwa watoto ndio chanzo kikubwa cha mimba za utotoni.
Pia Mushi katika Warsha hiyo aliataka wanawake kuwa na amri juu ya miili yao hasa katika suala zima la uzazi hali ambayo itapunguza umasikini katika familia zao na kuchangia haraka shughuli za maendeleo.
Mkurungezi wa TGNP Usu Mallya
alisema kuwa baada ya hitimisho la tamasha hilo la 11 washiriki
wote zaidi ya 2000 wanaoshiriki tamasha hilo kwa mwaka huu kutoka
mikoa mbali mbali Tanzania bara na visiwani watasaini tamko maalum
ambalo litaandaliwa na washiriki wa tamasha hilo kuhusu mchakato wa
katiba na tamko hilo litafikishwa katika bunge la katiba kama
mapendekezo ya wanawake nchini juu ya rasimu hiyo ya katiba.
CHANZO:matukiodaima.com