BAN KI MOON AMSHAURI RAIS KIKWETE KUHUDHURIA MKUTANO WA KAMPALA

Habari nilizopata hivi punde kutoka vyanzo vya kuaminika ni kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon kupitia kwa Mshauri wa UN katika ukanda wa Maziwa Makuu, Bi Mary ROBINSON, amemshauri Rais wa Tanzania JAKAYA KIKWETE kuhudhuria mkutano wa ICGLR unaofanyika Jijini Kampala, Uganda. Sababu zilizotolewa ni kama ifuatavyo

  1. Mkutano huo umepewa baraka zote za UN na kwamba umoja huo umetuma mwakilishi kuhudhuria kikao hicho ambaye ni Bi Mary Robinson
  2. Mkutano huo utajikita katika kujadili jambo moja tu ambalo ni hali ya amani mashariki mwa DRC na hautahusisha mazungumzo baina ya JK na PK kutokana na kupishana kauli katika siku za hivi karibuni.
  3. Kutokana na Tanzania kupeleka kikosi kupambana na waasi wa M23, Tanzania itapewa nafasi ya kuelezea mafanikio yaliyopatikana kutokana na operesheni hiyo na kwamba nchi zote za maziwa makuu zitatakiwa kuunga mkono juhudi za Tanzania
  4. Nchi washiriki watapewa makavu na Bi Mary Robinson kutokana na nchi hizo kuwa na tabia ya kuchochea migogoro DRC. Hapa walengwa wakubwa ni Rwanda na Uganda. itakumbukwa kuwa hivi karibuni Katibu Mkuu wa UN Ban Ki Moon amemshutumu Rais wa Rwanda PK kutokana na kusaidia waasi wa M23. Pia Afrika ya Kati inashutumiwa kusaidia waasi wa LRA.
  5. Usalama wa viongozi wote watakaohudhuria kikao hicho umeimarishwa na utakuwa ni jukumu la UN
  6. Tanzania kama nchi mama ya Maziwa Makuu, ni vema kuhudhuria mkutano huo kwa vile usalama wa nchi jirani unapozorota, ni Tanzania ndiyo inayoathirika hasa kupitia wimbi la wakimbizi, wahamiaji haramu na kuzagaa kwa silaha za kivita.
Kutokana na Mazungumzo hayo ambayo yamefanyika kwa njia ya simu baina ya Rais JK na Bi Mary Robinson, Rais JK amelazimika kusitisha ziara yake Mkoani Mwanza na kupanda ndege kuelekea Kampala Uganda jana jioni (tarehe 4/5/2013). Hivi tunavyozungumza Rais wetu amewasili salama na anahudhuria mkutano huo. Aidha, inaelezwa kuwa Rais wa Rwanda Paul Kagame mpaka leo asubuhi alikuwa hajathibitisha kuhudhuria na huenda asihudhurie kikao hicho ili kukwepa kibano cha Mwanamama Mary Robinson

CHANZO: JAMII FORUM


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo