YANGA KUUMANA NA MTIBWA SUGAR JUMAPILI HII

Mabingwa wa Ligi Kuu nchini msimu wa 2012/2013 timu ya Young Africans siku ya jumapili watashuka dimbani uwanja wa Taifa kucheza mchezo wa kirafiki wa kujipima nguvu na timu ya Mtibwa Sugar kutoka Manungu Turiani mjini Morogoro.

Akiongea na waandishi wa habari afisa habari wa klabu ya Yanga Baraka Kizuguto amesema watautumia mchezo huo kuwatambulisha wachezaji wake wote wapya waliosajiliwa kwa ajili ya msimu mpya wa Ligi Kuu ya Vodacom na mashindano ya kimataifa.

"Tumekua tukifanya mazoezi kwa takribani wiki mbili sasa, wachezaji waliokua na timu ya Taifa wamesharejea tayari na wameshaanza mazoezi leo pamoja na wachezaji wengine waliokuwepo hivyo kufanya kikosi kukamilika kwa sasa" alisema Kizuguto

Kocha mkuu Ernie Brandts aliyekuwa nchini Ujerumani kwa ajili ya masomo mafupi ya kuongeza muda wa leseni yake ya ukocha (UEFA Licence) anatarajiwa kurejea nchini siku ya jumamosi usiku na siku ya jumapili atakua pamoja na kikosi chake katika mchezo huo.

Wachezaji wapya waliosajiliwa na Yanga kwa ajili ya msimu huu wote wanatarajiwa kuwepo katika mchezo huo.

Wachezaji wapya waliosajiliwa msimu huu ni :
1. Deogratius Munishi 'Dida'  - Azam FC (golikipa)
2. Rajab Zahir - Mtibwa Sugar (mlinzi wa kati)
3. Hamis Thabit - Ureno (kiungo)
4. Shaban Kondo - Msumbiji (mshambuliaji)
5. Mrisho Ngassa - Azam (mshambuliaji)
6. Hussein Javu - Mtibwa Sugar (mshambuliaji)
7.  Reliants Lusajo - Machava FC (mshambuliaji)
Wakati huo huo Mweka hazina wa chama cha soka mkoa wa Dar es salaamm (DFRA) Ally Hassan ambao pia ndio waandaji wa mchezo huo amesema, taratibu zote za mchezo huo kati ya Yanga Vs Mtibwa Sugar zimekamilika na kila kitu kipo sawa kuelekea mchezo huo.

Viingilio vya mchezo huo ni:
VIP A - TSHS 15,000/=
VIP B & C - TSHS 10,000/=
Orange, Blue, Green TSHS 5,000/=


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo