Mwanamume
huyo mwenye umri wa zaidi ya miaka 50 alikamatwa Alhamisi jioni baada ya
kupatikana akifanya kitendo hicho katika kijiji cha Kigwandi, wilaya ya
Tetu.
Kaimu afisa
mkuu wa polisi katika eneo hilo, Bw Joseph Mwika alisema mwanawe
mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 10 alimuarifu kakake mkubwa baada ya
kumfumania babake akifanya kitendo hicho.
Bw Mwika alisema wawili hao walimripoti baba yao kwa chifu wa eneo hilo ambaye alimkamata na kumpeleka katika kituo cha polisi.
“Kuku huyo alikuwa wa mwanawe mwanamume huyo aliyeripoti kisa hicho kwa chifu,” alisema Bw Mwika.
Kuku huyo ambaye baadaye alikufa alipelekwa katika maabara ili kufanyiwa uchunguzi.
“Tunasubiri matokeo ya madaktari wa mifugo kabla ya kuchukua hatua,” afisa huyo alisema.