HII NDIYO MISHAHARA MIPYA YA WATUMISHI


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Celina Kombani.Dar es Salaam, Tanzania. Serikali awali ilitangaza mishahara mipya kwa watumishi wa umma na kufichwa, lakini sasa mishahara hiyo ya kila sekta mbalimbali imechapishwa kwenye gazeti moja la leo.

Kima cha chini kimeongezwa kwa asilimia 41.18  kutoka Sh170,000  mpaka Sh240,000 wakati mishahara ya watumishi wengine imeongezwa kwa wastani wa asilimia 8.41.

Waraka namba moja kwa watumishi wa umma kwa ajili ya mishahara hiyo ulitolewa na Katibu Mkuu, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, George Yambesi Julai 2, mwaka huu na kueleza kwamba marekebisho hayo yanahusu watumishi wa serikali kuu na watumishi wa serikali za mitaa.

Walimu

Katika sekta ya elimu, mshahara wa kima cha chini kwa walimu kimepanda kutoka Sh223,000 mpaka Sh296,000.

Wakaguzi

Mshahara kwa wakaguzi katika ofisi ya Taifa ya Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (SAIS) kima cha chini kimepanda kutoka Sh187,000 mpaka Sh249,000.

Sekta ya Kilimo

Mshahara katika sekta ya kilimo na mifugo kwa watafiti kima cha chini cha mshahara kimepanda kutoka Sh890,300 hadi Sh916,000.

Bunge

Kwa upande huo kima cha chini cha mshahara kimepanda kutoka Sh170,000 hadi Sh240,000.

Serikali Kuu

Upande wa wafanyakazi wa serikali kuu, mshahara wa kima cha chini umepanda kutoka 170,000 mpaka 240,000.

Mwanasheria Mkuu

Katika upande wa mwanasheria mkuu, kima cha chini cha mshahara kimepanda kutoka Sh310,000 hadi Sh360,000.

Mahakama

Hapa mshahara wa kima cha chini umepanda kutoka Sh469,000 hadi Sh510,000

Sekta ya Afya

Kwa wafanyakazi wa sekta ya afya nchini, mishahara kima cha chini imepanda kutoka Sh221,500 hadi Sh261,000.
Hiyo ni mshahara ya wafanyakazi wa umma kwa taarifa zaidi soma gazeti la mwananchi.

Chanzo: Mwananchi.


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo