HALMASHAURI YA WILAYA YA MAKETE YATANGAZA KIAMA KWA WAFUGAJI MAKETE MJINI

Halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe imetoa amri Kwa wafugaji waliopo makete mjini kuhakikisha wanafungia mifugo yao na kwa wale watakaokaidi mifugo yao itateketezwa kama sheria inavyosema

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo Bw. Iddi Nganya amesema sheria hairuhusu mifugo kuzurura ovyo mitaani maeneo ya mijini hivyo wamiliki wa mifugo hiyo wanatakiwa kutii sheria kwa kuifungia kwenye mabanda mifugo yao

Amesema mifugo inayoongoza kuzurura ovyo ni nguruwe, ng'ombe, mbwa na mbuzi ambapo wafugaji wamekuwa na kawaida ya kuiacha mifugo hiyo kuzurura ovyo mitaani na kusababisha bugudha kwa wananchi wengine ambao hawafugi mifugo hiyo ama ambao wameifungia mifugo yao

Zoezi la kuikamata na kuiteketeza mifugo hiyo litaanza jumatatu julai 22 mwaka huu, ambapo amewataka wananchi kutii sheria na kuifungia mifugo yao na kuacha mji ukiwa safi

Mei 20 mwaka huu Afisa kilimo mifugo na ushirika wa halmashauri hiyo Marietha Kasongo alitangaza kwenye kikao cha uwasilishwaji wa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za serikali wilayani Makete iliyosomwa na mkuu wa wilaya kuwa anatoa mwezi mmoja wafungaji wafungie mifugo yao lakini wapo waliokaidi na ndio maana zoezi hilo la kuikamata litaanza


JIUNGE NA EDMO BLOG SASA

Usipitwe!! Jiunge nasi kupitia Facebook,Twitter na Instagram ili kupata habari zote za town! Usikose kujiunga na Youtube kuangalia video zote kali kutoka Edmo Blog Pekee!, kujiunga bonyeza hapa>>>Youtube

Tupe Maoni Yako lakini Usiandike Matusi



 
© Copyright EDMO BLOG | Designed By Peruzibongo